Insta inayotumika kumtusi Diamond yaendelea kutoa matusi wakati mtuhumiwa mwenye akaunti yupo Selo | BONGOJAMII

Insta inayotumika kumtusi Diamond yaendelea kutoa matusi wakati mtuhumiwa mwenye akaunti yupo Selo

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
BONYEZA HAPA KU-DOWNLOAD

November 18, 2016 kijana mmoja ambaye jina lake halikutambulika mara moja alikamatwa na jeshi la polisi kwa tuhuma ya kutumia akaunti ya ‘Shilolekiuno_official’ kuwatukana watu mbalimbali akiwemo Diamond pamoja na familia yake.

Lakini cha kushangaza akaunti hiyo bado inaendelea kutukana watu wakati mtuhumiwa yupo ndani.


Sallam ambaye ni meneja wa Diamond ndiye aliyetoa taarifa za kukamatwa kwa kijana huyo mwezi Disemba mwaka jana.


“Kwa watu wote kama ulitukanwa na huyu ambae anaejiita @shilolekiuno_official kwa sasa yupo chini ya mikono ya sheria, Kama una mashitaka yoyote fika Oyster Bay Polisi, Vizuri ametaja watu wanaemtuma afanye hivyo! Na kuwasaidia wale ambao wanajiamini kuwa hawawezi kujulikana basi kwa taarifa yenu Serikali ina mkono mrefu sana! Eti Jana alikuwa anamuita Diamond “Simba” 😂😂😂.”aliandika Sallam Insta baada ya kukamatwa kwa jina hiyo.

Hata hivyo kamanda wa polisi wa Kinondoni, Suzan Kaganda alikiambia kipindi cha Planet Bongo cha EA Radio kuwa hakuna kijana kama hiyo aliyekamatwa.


“Hatujamkamata na hatuna mtu kama huyo kituoni kwetu. Tuna vijana wengi ambao wamekamatwa wanamakosa kama hayo, jina kama hilo uliloniuliza halipo hapa kituoni kwetu labda kwenye kituo kingine.”

Hii ni baadhi kati ya post mpya za kwenye akaunti hiyo.
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka

Featured Posts