Pichazz: Hivi Ndivyo Mshiriki wa BSS ,Miriam Alivyomwagiwa Mikojo Wakati wa Kusherekea Sikuku Yake Ya Kuzaliwa. | BONGOJAMII

Pichazz: Hivi Ndivyo Mshiriki wa BSS ,Miriam Alivyomwagiwa Mikojo Wakati wa Kusherekea Sikuku Yake Ya Kuzaliwa.

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
BONYEZA HAPA KU-DOWNLOAD
RICHARD BUKOS, RISASI
DAR ES SALAAM: Mwa n amu z i k i wa Taarab, Mar­iam Mohammed Uwesu ‘Mariam BSS’ Jumapili aliyopita alijikuta akimwagiwa kojo wakati wa sherehe ya kum­bukumbu ya siku yake ya kuzaliwa ‘bethidei’ iliyofan­yika huko Manzese katika baa inayojulikana kama Bar Mpya, jirani na Friends Cor­ner Hotel.


Katika hafla hiyo iliy­osindikizwa na Kundi la Taarab la Diamond Clas­sic Modern usiku huo, mshiriki huyo wa zamani wa shindano la kusaka vi­paji la BSS, alimwagiwa pombe, maji machafu, soda na ndoo ya chooni iliyokuwa na mikojo wakati wa tukio la kufungua shampeni, am­balo kwa desturi mpya ya sasa, mhusika humwagiwa kinywaji hicho, sambamba na maji na vinywaji vingine laini.

Mambo yalienda vizuri hadi mshereheshaji ka­tika tukio hilo, Mc An­damakopa alipotangaza kuwa wakati wa kufun­gua shampeni umefika na mara tu baada ya kinywaji hicho kufunguli wa, wageni wa alikwa walianza kummwa­gia kwa staili ya kumuogesha.

Kitendo hicho kiliamsha shamra kwa watu walioku­wepo, wakiwemo ‘masela’ ambao nao walimvamia na kuanza kummwagia vimim­inika mbalimbali zikiwemo pombe kali, soda na maji machafu.

Wakati hayo yakiende­lea, wanaosadikika kuwa masela, walienda chooni na kuchukua ndoo ya maji yali­yochanganyika na mikojo na kwenda kummwagia mwilini hali iliyosababisha baadhi ya wasamaria wema kumcho­moa katikati ya kundi hilo baada ya kushtukia harufu kali ya mkojo.

Baada ya kuchomolewa alikimbizwa chooni kwenda kuoga ndipo mambo men­gine yakaendelea huku mwanamuziki huyo akiwala­lamikia waliomfanyia kiten­do hicho akisema hakikuwa cha kiungwana.

“Ukweli suala la kumwa­giana shampeni au maji ni la kawaida, lakini kitendo walichonifanyia cha kun­imwagia maji machafu yanayonuka harufu ya mikojo si cha kiungwana.

“Ile ndoo wa­meitoa chooni na si unajua vyoo vya baa, walevi wengine wak­ienda kukojoa hawaangalii, wanakojolea hata maji ya kunawa , ” alilalamika Mariam.
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka

Featured Posts