Serikali Yafunguka Juu ya Hali ya Njaa Nchini,Huu Ndio Uamuzi Uliotolewa Kuikabili Hali Hiyo..!!! | BONGOJAMII

Serikali Yafunguka Juu ya Hali ya Njaa Nchini,Huu Ndio Uamuzi Uliotolewa Kuikabili Hali Hiyo..!!!

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
BONYEZA HAPA KU-DOWNLOAD



Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali imeruhusu tani milioni 1.5 za chakula zilizokuwa zimehifadhiwa zianze kuuzwa ili kukabiliana na kupanda kwa bei za vyakula.



Pia, Majaliwa amesema kupanda kwa bei ya vyakula nchini kulichangiwa na ukosefu uliojitokeza nchi jirani, lakini akawataka wananchi wasiwe na hofu kwani chakula kipo cha kutosha.


Kauli ya Waziri Mkuu imekuja wakati mjadala wa upungufu wa chakula nchini ukizidi kupamba moto na kusababisha baadhi ya wadau kudai kuwa, Serikali inachelea kutangaza kuwa kuna njaa nchini.


Tayari, Rais John Magufuli ameshaeleza kuwa hakuna baa la njaa na kama litatokea, yeye ndiye pekee mwenye mamlaka ya kutangaza na kufafanua kuwa tatizo hilo linakuzwa na wafanyabiashara wachache na wanasiasa wanaotaka kujinufaisha na hali hiyo.


Jana, Majaliwa aliyezungumza na waandishi wa habari baada ya kuwasili mjini hapa na ndege ya kwanza ya Bombadier kufanya safari za kibiashara kati ya Dar es Salaam na Dodoma, alisema hali ya upatikanaji chakula nchini ni tofauti na inavyoelezwa na baadhi ya vyombo vya habari.
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka

Featured Posts