Update: Chanzo cha moto Uwanja wa Ndege wa JNIA, Dar chajulikana | BONGOJAMII

Update: Chanzo cha moto Uwanja wa Ndege wa JNIA, Dar chajulikana

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
BONYEZA HAPA KU-DOWNLOAD

DAR ES SALAAM: Moto mkubwa umezuka kwenye Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere (JNIA) usiku wa leo na kusababisha taharuki kubwa kwa wasafiri na watumiaji wa uwanja huo, ambapo imelazimu shughuli zote uwanjani hapo kusitishwa kwa muda wakati vikosi vya zimamoto vikiendelea na kazi yao kwenye uwanja huo mkubwa zaidi nchini Tanzania.


Kamanda wa Polisi wa Viwanja vya Ndege, Martin Otieno ameuambia mtandao huu kuwa wamefanikiwa kuudhibiti moto huo na kwamba uchunguzi wa kina juu ya chanzo cha moto huo na hasara iliyosababisha, unaendelea kufanyika na kwamba tayari shughuli zote za kawaida zinaendelea kama kawaida.


Aidha Meneja wa Uwanja huo ameeleza kuwa kwa sasa shughuli zote za usafirishaji zimeamishiwa Terminal One na zinaendelea kama kawaida huku wakiweka sawa maeneo yalioathirika.


“Kwanza naomba niwatoe hofu Watanzania na wasafiri wote wanaotumia Uwanja wetu, ni kweli moto umezuka kuanzia majira ya saa 6 hadi saa 7 usiku wa kuamkia leo.


“Lakini madhara kidogo yametokea kwenye jengo la kuhifadhia mizigo pekee, hakuna mtu aliyepoteza maisha wala kujeruhiwa kutokana na moto, na sasa shughuli zote za usafirishaji tumezihamishia kule terminal one (Uwanja wa zamani) zinaendelea kama kawaida”. Amesema Meneja huyo.


“Baada ya kuudhibiti moto huo tumerudi kuangalia chanzo tukakuta, mfumo wa umeme uko sawa, hivyo hatujajua chanzo hasa cha moto huo ila tunajitahidi kufanya utafiti ili tujue.” Aliongeza Meneja na kusema taarifa zaidi, zitatolewa baadaye.

Raia akichukua picha za tukio hilo huku walinzi wakitaharuki.

Vikosi vya ulinzi na usalama vikiwasili eneo la tukio.

Wasafiri wakitaharuki kuona moto huo ukizuka na kusababisha taharuki kubwa miongozni mwao.



Moto ukiwaka viwanjani hapo.


UPDATES: CHANZO CHA MOTO UWANJA WA NDEGE DAR CHAJULIKANA


Taarifa zilizotufikia hivi punde zimeeleza kuwa, chanzo cha moto mkubwa uliozuka usiku wa kuamkia leo kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), jijini Dar es Salam na kusababisha shughuli zote za usafirishaji Uwanjani hapo kusimama kwa muda, kimejulikana kuwa ni hitilafu ya umeme.


Akizungumza na mtandao wa Global Publshers mapema asubuhi ya leo, Kamanda wa Polisi wa Viwanja vya Ndege, ACP Martin Otieno amesema kuwa, uchunguzi umebaini kwamba, kulikuwa na tatizo la umeme ambalo hata hivyo lilishughulikiwa mara moja.


“Kulikuwa na tatizo la umeme kwenye eneo la kuhifadhia mizigo lakini moto ulidhibitiwa vizuri na sasa shughuli zinaendelea kama kawaida japokuwa bado tunatumia Terminal One (uwanja wa zamani) kwa kuwabeba abiria kwenye mabasi na kuwapeleka panapohusika.


“Kwa sasa ndege zote zinatua na kuruka bila tatizo lolote na kufuatana na ratiba hivyo hakuna hofu yoyote kwani muda si mrefu eneo hilo la mizigo litakuwa limeshawekwa sana, ” alisema Kamanda Otieno.


Aidha Mamlaka ya Uwanja huo imetoa mabasi kwa ajili ya kubeba abiria kuwapeleka Terminal One ambako shughuli za usafirishaji zinaendelea kama kawaida.
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka

Featured Posts