Baada ya Sekeseke la Madawa ya Kulevya Kutulia,TID Aamua Kumtaja Tena Diamond.. | BONGOJAMII

Baada ya Sekeseke la Madawa ya Kulevya Kutulia,TID Aamua Kumtaja Tena Diamond..

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
BONYEZA HAPA KU-DOWNLOAD


Kwa sasa msanii TID Mnyama anahakikisha anarudisha makali yake ya zamani kwenye muziki. Muimbaji huyo amewaahidi mashabiki wake kufanya kazi na Diamond hivi karibuni.


Akiongea kwenye kipindi cha XXL, kupitia Clouds FM Ijumaa hii, Mnyama amesema kuna nyimbo anayofikiria kumshirikisha Diamond ambaye taarifa hizo tayari ameshazipata.


“Nina ngoma nafikiri itafaa zaidi nikimshirikisha Diamond. Diamond ameshapata habari nafikiri tutaifanya ngoma hiyo soon as possible,” amesema TID.


Kwa sasa msanii huyo ameachia wimbo wake mpya aliomshirikisha rapper Fid Q unaojulikana kama ‘Maisha ya Jela’ pamoja na mwingine uitwao Woman.
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka

Featured Posts