Wanafunzi 4 wa Chuo Kikuu cha Kampala Kortini kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kupitia WhatsApp. | BONGOJAMII

Wanafunzi 4 wa Chuo Kikuu cha Kampala Kortini kwa Kumkashifu Rais Magufuli Kupitia WhatsApp.

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
BONYEZA HAPA KU-DOWNLOAD


Wanafunzi wanne wa Chuo Kikuu cha Kampala(KIU) kampasi ya Dar es Salaam, wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala, kujibu shitaka la kusambaza picha za kumkashifu Rais John Magufuli kupitia mtandao wa kijamii wa WhatsApp.


Washitakiwa hao ni Amenitha Kongo(19), Maria Tweve (20), Agnes Gabriel(21) na Anne Mwansasu(21), ambapo wamepandishwa mahakamani hapo leo na kusomewa shtaka linalomkabili mbele ya Hakimu Mkazi Catherine Kiyoja.


Kwa pamoja washtakiwa hao wanadaiwa kuchapisha picha ambazo zinaonyesha Rais Magufuli akiwa amevaa hijabu kama mwanamke wa Kiislamu na kuzisambaza kwenye mtandao huo wa WhatsApp, huku wakijua kufanya hivyo ni kinyume cha sheria.


Washtakiwa wamerudishwa rumande baada ya kushindwa kitimiza masharti ya dhamana.
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka

Featured Posts