KOREA KASKAZINI YATOA MAKOMBORA FEKI | BONGOJAMII

KOREA KASKAZINI YATOA MAKOMBORA FEKI

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
BONYEZA HAPA KU-DOWNLOAD
Korea Kaskazini imelaumiwa kwa kuonyesha silaha bandia katika maonyesho ya hivi karibuni ya ubabe wake wa kijeshi.

Afisa wa zamani wa masuala ya ujasusi anasemna baadhi ya bunduki na makombora yaliyotumiwa kwenye maonyesho hayo yalikuwa bandia.

Michael Pregent alikiambia Kituo cha Runinga cha Fox kuwa baadhi ya bunduki zilizokuwa kwenye maonyesho hayo zilikuwa ni za bandia (magumashi). Lakini maonyesho kama hayo kuonyesha ubabe wa kijeshi yametumiwa kwa miongo kadhaa.

Kwa sasa msukosuko ni mkubwa kati ya Marekani na Korea Kaskazini. Hii ni baada ya rais wa Marekani, Donald Trump kuapa kuwa ni lazima atakabiliana na vitisho vya Korea Kaskazini.

“Sio kuwa Korea Kaskazini inafikiri kuwa itashinda Marekani lakini kile itafanya ikiwa itashambuliwa,” Pregent alisema.

Silaha hizi bandia zilitengenezwa kukwepa mashambulizi ya angani na kuwachanganya marubani ya jeshi kushambulia vifaru bandia baada ya vifaru halali

Wasanii wa jeshi la Ufaransa nao walichora mito bandia na mitaro ili kuwachanganya marubani wa ndege za vita. Ujanja kama huo pia ulitumiwa wakati wa vita vya pili vya Dunia

Miti hii ilipakwa rangi hadi kifanana na silaha ya kurusha makombora. Lengo lilikuwa ni kuwachanganya maadui kuhusu ni wapi kulikuwa na adui. Aina hii ya silaha bandia zilitumika karne za 18 na 19.

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka

Featured Posts