WATU 13 WAPOTEZA MAISHA KWENYE AJALI | BONGOJAMII

WATU 13 WAPOTEZA MAISHA KWENYE AJALI

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
BONYEZA HAPA KU-DOWNLOAD

Watanzania 13 wamefariki na wengine nane kujeruhiwa katika ajali iliyotokea usiku wa kuamkia leo katika eneo la biashara Lubanda takribani kilomita 80 kufika kituo cha polisi cha Fika salama karibu na Mto Katonga wilaya ya Mpigi huko Kampala, Uganda.


Ajali hiyo imehusisha gari aina ya fuso yenye namba za usajili UAH 970P na coaster yenye namba T540 DLC waliokuwa wakitumia watu hao wakiwemo watanzania ambao inasemekana walikuwa wakitoka kwenye harusi ya binti wa Dkt. Annette Ibingira ambaye ni mke wa mhazini wa shule ya Wazazi ya Kampala nchini Uganda Dkt. Ibingira.


Majeruhi wa ajali hiyo wamepelekwa katika hospitali ya Nkozi pamoja na Double Cure Clinic zilizopo nchini Uganda huku miili ya watu waliopoteza maisha katika ajali hiyo imepelekwa hospitali ya Gombe kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi nchini humo.

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka

Featured Posts