Adhabu za kikatili mashuleni zapigwa marufuku.. | BONGOJAMII

Adhabu za kikatili mashuleni zapigwa marufuku..

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
BONYEZA HAPA KU-DOWNLOAD

Serikali imepiga marufuku tabia ya baadhi ya waalimu kutoa adhabu kali na za kikatili kwa wanafunzi na badala yake waalimu wameelekezwa kutoa adhabu kulingana na taratibu na sheria zilizowekwa.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. George Simbachawene kupitia hotuba yake iliyosomwa na Mkurugenzi Msaidizi kutoka Ofisi ya Rais katika uzinduzi wa ripoti ya elimu ya msingi nchini amesema, kumekuwa na tabia ya baadhi ya waalimu kutoa adhabu kinyume cha taratibu.


Naye Mratibu wa Mtandao wa Elimu nchini ambao ni wasimamizi wa utafiti huo Bi. Cathrene Sekwao na mtafiti Bw. Jacob Kateri amesema wameamua kufanya utafiti huo ili kuweza kujua hali ya elimu ikoje ili serikali iweze kuona nini kifanyike kuboresha sekta ya elimu ambapo pia wameitaka serikali kupitia mapendekezo yao.
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka

Featured Posts