DIAMOND AMFUTA MACHOZI MZAZI MWENZAKE BAADA YA KIFO CHA IVAN DON | BONGOJAMII

DIAMOND AMFUTA MACHOZI MZAZI MWENZAKE BAADA YA KIFO CHA IVAN DON

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
BONYEZA HAPA KU-DOWNLOAD
Diamond Platnumz ametuma ujumbe wa kumfariji mama watoto wake wake, Zari, kufutia msiba mzito wa Ivan ambaye ni baba watoto watatu wa Zari.

Diamond akiwa na Zari pamoja na watoto wa marehemu, Ivan. Picha hii ni yazamani

Kumekuwa na mengi yanazungumzwa kwenye mitandaoni ya kijamii kuhusu Zari, Ivan na Diamond Platnumz na mengine yamepelekea kuwakera baadhi ya mashabiki wao wa damu.

Diamond ameandika ujumbe wa kumtia moyo Zari The Boss Lady na kuonyesha yupo naye pamoja katika kipindi hicho kigumu anachopitia.

“Natamani ningekukumbatia badala ya kukutumia sms,najua upo kwenye wakati mgumu na ni mpweke, jua kwamba hauko mwenyewe, niko na wewe hapa usiku na mchana,” aliandika Diamond Instagram.

Ivan amefariki dunia Alhamisi hii nchini Afrika Kusini baada ya kuugua ugonjwa wa moyo kwa wiki kadhaa.

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka

Featured Posts