ZITTO KABWE AFUNGUKA KUHUSU UTAFITI WA TWAWEZA | BONGOJAMII

ZITTO KABWE AFUNGUKA KUHUSU UTAFITI WA TWAWEZA

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
BONYEZA HAPA KU-DOWNLOAD
Twaweza leo August 30, 2017 imetoa ripoti ya matokeo ya utafiti mpya kuhusiana na masuala ya huduma za afya ambayo inaonesha kuwa 70% ya wananchi wanaokwenda kwenye vituo vya kutolea huduma za afya hawapati dawa na vifaa tiba vya kutosha changamoto ambayo imeongezeka kutoka 62% mwaka 2015.

Akizungumza kuhusiana na matokeo hayo Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi wa ACT Wazalendo Zitto Kabwe amesema lipo tatizo kubwa katika masuala ya afya ukizingatia kuwa Bajeti ya Serikali katika dawa imengozeka hivyo Wizara ya Afya inawajibika kutolea ufafanuzi jambo hilo na kutafuta njia ambayo itamaliza changamoto hii.

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka

Featured Posts