MAN U WAMUWEKEA NEYMAR DAU KUBWAA, JE ATACHOMOKA?? | BONGOJAMII

MAN U WAMUWEKEA NEYMAR DAU KUBWAA, JE ATACHOMOKA??

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
BONYEZA HAPA KU-DOWNLOAD
Manchester United imepania kuhakikisha inamsajili nyota wa Barcelona, Neymar Jr kipindi cha kiangazi baada ya kuanzisha mazungumzo ya awali.


Hata hivyo, mchezaji huyo amekuwa akionyesha waziwazi mapenzi yake kwa timu yake ya sasa ya Barcelona, jambo ambalo limewafanya Manchester United kuingia mfukoni na kutangaza dau kubwa ambalo litamshawishi Neymar.


Licha ya kwamba Mashetani hao wekundu wa London wametangaza kufanya kufuru ya usajili wa dunia kwa kulipa fedha ya uhamisho wa Pauni 170 ili kuipata huduma yake, lakini mchezaji huyo bado amekuwa akisisitiza kwamba anafurahia maisha akiwa na miamba hiyo ya Hispania.


Hilo limetokana na Neymar kufurahia muunganiko wa Lionel Messi na Luis Suarez wanapokutana wachezaji hao watatu na kuunda kikosi hatari maarufu MSN ambacho kimekuwa tishio kwa mabao.

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka

Featured Posts