TID ALALAMIKA KUTOSWA NA RAFKI ZAKE | BONGOJAMII

TID ALALAMIKA KUTOSWA NA RAFKI ZAKE

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
BONYEZA HAPA KU-DOWNLOAD


Msanii wa muziki wa kizazi kipya TID Mnyama amefunguka na kusema sasa hivi watu ambao mwanzo walikuwa wakimpa support kwenye muziki na mambo yake mengine wamemtosa na hawampi msaada wowote hivyo kila kitu anapambana mwenyewe. 


TID amesema hayo kwenye kipindi cha Planet Bongo ya East Africa Radio na kusema watu hao wameacha kumpa suport baada ya yeye kuachana na madawa ya kulevya hivyo saizi wao wanamuona yeye ni kama msaliti.


"Saizi kila kitu nafanya mwenyewe hata hao mabrother unaosema washanitosa maana wao walikuwa wanapenda kuona nazidi kuharibika, hivyo toka nimetangaza kuachana na madawa ya kulevya wao wananiona mimi kama 'snitch', lakini hilo halina tatizo kwani mimi mwenyewe niko vizuri ndiyo maana unaweza kuona video hii nimetumia pesa nyingi kuifanya na nimelipa mwenyewe, hii pesa ningesema ninue gari basi ningepata Mark X nyingine lakini nimeamua kuiweka kwenye video ili kuleta ubora zaidi" alisema TID 


TID leo ameachia ngoma yake mpya inayokwenda kwa jina la 'Woman' na kusema siku yoyote ataachia video ya ngoma.

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka

Featured Posts