SERIKALI YAZUIA PASSPORT ZA VIGOGO HAWA WA MCHANGA WA MADINI | BONGOJAMII

SERIKALI YAZUIA PASSPORT ZA VIGOGO HAWA WA MCHANGA WA MADINI

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
BONYEZA HAPA KU-DOWNLOAD
Serikali imeagiza, Mawaziri, Wanasheria Wakuu wa Serikali na Manaibu wao, Wakurugenzi wa idara za mikataba, na Makamishna wa madini, wanasheria wa Wizara ya Nishati na Madini na watumishi wengine wa Serikali na watu wote waliohusika katika kuingia mikataba ya uchimbaji madini, utoaji wa leseni za uchimbaji wa madini na kuongeza muda wa leseni, watumishi na wamiliki wa makampuni ya madini kuto toka nje ya mipaka ya Tanzania.

Agizo hilo lilitolewa jana na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba ambaye alisema kuwa, wote waliotajwa kuhusika katika kulisababishia taifa hasara kupitia sekta ya madini, hawaruhusiwi kutoka nje ya mipaka ya Tanzania isipokuwa kwa kibali maalum kutoka serikalini.

“Naelekeza wote waliotajwa kuhusika hakuna kutoka nje ya mipaka ya nchi yetu isipokuwa kwa kibali maalum kutoka serikalini. Vyombo vitekeleze maagizo ya Rais kwa utimamu,” aliandika Waziri Nchemba kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii.

Agizo hili limekuja ikiwa ni saa chache tangu Rais Magufuli alipoagiza kuwa, viongozi wote na watumishi mbalimbali waliohusika katika kusaini mikataba mibovu na kushiriki kwa namna yoyote ile, wahojiwe.

Miongoni mwa watakaoathiriwa na zuio hilo, ni pamoja na Maafisa wa TRA, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Andrew Chenge, Mwanyika, na Werema, Mkurugenzi Idara ya Mikataba, Mary Ndosi, Kamishna Dalali Peter Kafumu, Waziri Prof. Muhongo, Waziri Daniel Yona, Waziri Nazir Karamagi, Jaji Julius Malaba, Waziri William Ngeleja.

Awali Waziri Nchemba alimpongeza Rais Magufuli kwa jitihada alizozichukua katika kuhakikisha analinda rasilimali za wanyonge na kusema kuwa hakuna uzalendo kama huo.

“Hakuna uzalendo zaidi ya kulinda rasilimali za Taifa, Hakuna utetezi wa wanyonge zaidi ya kulinda rasilimali zao.Hongera sana Mh.Rais kwa uzalendo wa vitendo kwa Taifa letu.”

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka

Featured Posts