BRAZIL YAISAMEHE TANZANIA DENI LA BILLION 445 | BONGOJAMII

BRAZIL YAISAMEHE TANZANIA DENI LA BILLION 445

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
BONYEZA HAPA KU-DOWNLOAD

Serikali ya Brazil imeisamehe Tanzania deni Dola 203milioni ambazo sawa Bilioni 445 ambalo limetokana na mkopo uliotolewa kwaajili ya ujenzi wa barabara ya Morogoro-Dodoma mwaka 1979.

Balozi wa Tanzania Nchini Brazil Dk Emmanuel Nchimbi amesaini mkataba huo kwaniaba ya Tanzania huku Wakili wa Hazina ya Taifa Dk Sonia Portella Nunes akisaini kwa niaba ya Serikali ya Brazil.

Balozi Nchimbi ameishukuru Serikali ya Brazil kwa msamaha huo ambao amesema umeunga mkono jitihada za Rais Dk. John Magufuli kujenga uchumi imara wa Tanzania.

Balozi Nchimbi pia ameuhakikishia Serikali ya Brazil utayari wa Tanzania katika kuimarisha ushirikiano wa kibiashara na uchumi na Brazil.

Hivyo kuanzia sasa kampuni za Brazil zinaruhusiwa kukopa katika Benki za Brazil kwa ajili ya kutekeleza miradi nchini Tanzania lakini pia Serikali ya Tanzania inaruhusiwa kuanzisha majadiliano ya miradi mipya ya maendeleo.

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka

Featured Posts