SIRO AKOMAA NA WENYE TUHUMA ZA MADAWA YA KULEVYA, AWATAKA WAFIKE KITUONI | BONGOJAMII

SIRO AKOMAA NA WENYE TUHUMA ZA MADAWA YA KULEVYA, AWATAKA WAFIKE KITUONI

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
BONYEZA HAPA KU-DOWNLOAD
Dar es Salaam. Kamishina wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam Simon Sirro amewataka wote walioitwa polisi ili kuhojiwa kwa tuhuma za dawa za kulevya, wafike kituoni hapo mara moja.

Kamishina Sirro amesema hayo leo (jumatano) wakati akizungumza na waandishi wa habari ambapo amesema ni vyema watu hao wakaripoti ili kama hawana hatia wasafishwe au wakikutwa na hatia wapelekwe mahakamani kwa ajili ya taratibu nyingine za kisheria.

"Niwaombe waliopokea wito wa polisi waje wahojiwe kwa sababu mtu akija mwenyewe inasaidia tofauti na anaposubiri nguvu ya dora kutumika kumkamata ambapo lolote linaweza kutokea hasa kwa yule anayekataa hata kukamatwa." amesema Siro

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka

Featured Posts