STAA WA AFRIKA KUSINI ALIYEKUA NA TATIZO LA KUKUA HARAKA ONTLAMETESE PHALATSE AFARIKI DUNIA | BONGOJAMII

STAA WA AFRIKA KUSINI ALIYEKUA NA TATIZO LA KUKUA HARAKA ONTLAMETESE PHALATSE AFARIKI DUNIA

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
BONYEZA HAPA KU-DOWNLOAD
Staa wa nchini Afrika Kusini aliyekuwa akipendwa kutokana na kuwa mwenye furaha licha ya tatizo la kukua haraka alilokuwa nalo, Ontlametse Phalatse amefariki dunia.

Amefariki jana usiku kwenye hospitali ya Dr George Mukhari Academic huko Ga-Rankuwa, Pretoria. Phalatse aliyekuwa na miaka 18, alikuwa mmoja kati ya wasichana wawili tu nchini humo wenye tatizo hilo nadra liitwalo Progeria.

Awali madaktari wake walitabiri kuwa angekuwa hadi akifikisha miaka 14 tu. Mwezi uliopita Rais Jacob Zuma alitimiza ndoto ya msichana huyo kuonana naye.

Taarifa ya familia yake imesema: It is with great sadness to inform you of the passing of our first lady, Ontlametse Ntlami Phalatse. Our hearts are filled with pain and sadness but Ontlametse — as we know her — would want us to carry on with her courageous spirit.”

Alikuwa maarufu sana Instagram ambako alikuwa na followers 63.6k.
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka

Featured Posts