WOLPER ADAI ANAKOMOLEWA KWENYE MAPENZI | BONGOJAMII

WOLPER ADAI ANAKOMOLEWA KWENYE MAPENZI

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
BONYEZA HAPA KU-DOWNLOAD
Malkia wa filamu, Jacqueline Wolper amefunguka kueleza moja na sababu ya mahusiano yake na wanaume wengi kushindwa kudumu kwa muda mrefu.

Muigizaji huyo ambaye ameachana na msanii Harmonize miezi kadhaa iliyopita, amedai kuna baadhi ya wasichana wanaingilia mapenzi yake ili kumkomoa.

“Mimi ni kama nina kipaji cha kukomeshwa kwenye mapenzi kwa sababu kipaji ninachokivumbua mimi wenzangu wanataka wapite hapo hapo ili kunikomoa. Ni kwamba nina kipaji cha kukomeshwa lakini huyo anayenikoa unakuta hajui mimi nimepambana vipi kumtengeneza mtu anipendae” alisema Wolper.

Licha ya Wolper na Harmonize kutoweka wazi sababu ya kuachana, lakini stori ambazo ziko mtaani zinadai Harmonize amemuacha muigizaji huyo baada ya kupata mwanamke wakizungu.

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka

Featured Posts