RAIS MAGUFULI AFANYA UTEUZI HUU APA | BONGOJAMII

RAIS MAGUFULI AFANYA UTEUZI HUU APA

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
BONYEZA HAPA KU-DOWNLOAD
Rais John Pombe Magufuli

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jonh Pombe Magufuli, amefanya uteuzi wa viongozi mbali mbali akiwemo Mkuu wa chuo kikuu cha Ardhi.

Taarifa rasmi iliyotolewa na Ikulu jijini Dar es salaam inasema Rais Magufuli amemteua Prof. Evaristo Liwa kuwa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ardhi, kuchukua nafasi ya Prof. Idrissa B. Mshoro ambaye amestaafu.

Wakati huo huo Rais Magufuli amewateua Prof. Abdulkarim Khamis Mruma kuwa Mwenyekiti wa kampuni ya kuhifadhi mafuta (TIPER), ambaye kabla alikuwa ni Mtendaji Mkuu wa wakala wa Jiologia Tanzania, na Prof. Joseph Buchweshaija kuwa Mwenyekiti wa Kampuni ya Puma Energy Tanzania LTD.

Prof. Buchweshaija alikuwa Naibu Mkuu wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es salaam (DUCE).


Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka

Featured Posts