RAIS MAGUFULI ATANGAZA VITA NA WALIOGUSHI UMRI | BONGOJAMII

RAIS MAGUFULI ATANGAZA VITA NA WALIOGUSHI UMRI

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
BONYEZA HAPA KU-DOWNLOAD
RAIS John Magufuli amesema serikali inawachunguza watumishi wa umma waliogushi umri ili wasibaki kwenye utumishi wa umma kwa muda ambao hawakustahili kuwa kazini.

Kadhalika, amesema kuna watumishi wenye miaka 60 na zaidi ambao hawataki kustaafu huku waking’ang’ania ajira na madaraka, na wengine wakijipachika vyeo vya ukurugenzi.

Akizungumza katika sherehe za maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani (Mei Mosi) ambazo kitaifa zilifanyika jana katika Viwanja vya Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi, Rais Magufuli alisema uchunguzi huo wa umri umeshaanza.

“Wako watumishi ambao wamebadilisha umri wao," alisema Rais Magufuli. "Wamebadilisha miaka yao na unakuta ni mzee kabisa, lakini kabadilisha umri."
"Kuna watu ambao ni wazee tena kuliko mimi. Wanasema hawaondoki eti ndio wakati umefika, hao nao tunawachunguza.”

Katika hotuba yake, Rais Magufuli alisisitiza kuwa wapo watumishi wa umma ambao bado wanafanya kazi wakiwa wameshatimiza umri wa kustaafu kwa lazima wa miaka 60 lakini hawataki kustaafu ili kuachia nafasi wegine waajiriwe.

Uchunguzi huo unakuja siku chache baada ya serikali kufanya uhakiki wa vyeti vya elimu vya wafanyakazi wake na kugundua takriban watumishi 10,000 wana vyeti vya kughushi. Wamefukuzwa kazi mara moja.

Akionyesha kukerwa na hali hiyo Rais Magufuli alisema:

“Sheria za nchi yetu hazijasema mtu anayetakiwa kufanya kazi lazima awe na digrii, kila kazi ina qualification (sifa) zake.

"Haiwezekani Watanzania wote wakawa na digrii, darasa la saba wanaajiriwa, form four (kidato cha nne) wanaajiriwa na wenye certificate (cheti) wanaajiriwa.

"Na kila mmoja ana wajibu wa kuajiriwa.

”Tunachosisitiza hapa kama wewe ni darasa la saba na unataka kuajiriwa kaombe kazi ya darasa la saba, kama wewe ni form four kaombe kazi ya form four, kama una certificate nenda ukaombe kazi ya certificate. Usiende ukatafute mavyeti ya kufoji ukajiita daktari kumbe hata unesi haujafikia,”alisema
Aidha, Rais Magufuli alisema wako watumishi ambao wamekuwa wakijiita wakurugenzi, "watu wakubwa wakubwa tu, wana mavyeti ya kufoji, halafu wanawanyanyasa hawa watu wa chini ambao wana vyeti halali."

Alisema kundi hilo nalo ni miongoni mwa watumishi wa umma ambao serikali imekuwa ikiwaamini lakini imegundua kumbe hawastahili nafasi hiyo.

Mbali na kuahidi kushughulikia watumishi walioghushi umri ili kufanya kazi nje ya miaka ya kustaafu, Rais Magufuli alistahili kurejesha nyongeza ya kila mwaka ya mishahara na upadishaji watumishi madaraja.

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Bongojamii Blog kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka

Featured Posts